• We are Located near Skanda Secondary School, Mwinyi Street - Tabora

Ifahamu Idara ya Watoto


Idara ya Watoto na Wanafunzi ni Idara ndani ya kanisa la TAG, lilianzishwa rasmi Mwaka 1994 kufuatia mkutano wa viongozi wa Kanisa la Assemblies of God, barani Afrika, “Africa Assemblies of God Alliance” (AAGA) uliofanyika Nairobi, nchini Kenya mwaka mwaka 1993. Idara hii ilianzishwa ikiwa ni utekelezaji wa maazimio muhimu katika mkutano huo wa (AAGA). Mwaka huo wa 1994 kanisa la TAG lilikuwa linaongozwa na Askofu Mkuu Rev. Ranwell Mwenisongole na alimteua marehemu Mchungaji Joseph Justine kuwa Mkurugenzi Mkuu. Kadhalika, marehemu Mchungaji Jeremiah Kimaro aliteuliwa kuwa Makamu Mkurugenzi Mkuu na Mch. Everhard Mloka kuwa Katibu Mkuu. Huo ndio ukawa mwanzo mzuri wa Idara hii.

MaonoKuwafanya watoto wa Tanzania kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, waliojazwa Roho Mtakatifu na kuukulia Wokovu, hatimaye wawe watoto bora kwa wazazi na jamii, hivyo kuwa viongozi wa kanisa na Taifa la Kesho.

MaadiliUbora na Uaminifu kwa Mungu ni dira bora kwa watoto. Kimsingi watoto ni binadamu wenye viungo vyote na ufahamu wote ila wasioweza kujitegemea, Hivyo tunawekeza waweze kuandaliwa ipasavyo.